Psalms 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 aWale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.

2 bKama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.


3 cFimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi
waliopewa wenye haki,
ili wenye haki wasije wakatumia
mikono yao kutenda ubaya.


4 dEe Bwana, watendee mema walio wema,
wale walio wanyofu wa moyo.

5 eBali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,
Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.
Copyright information for SwhKC